Saturday, March 16, 2013

Neno la leo

Mk 6:34 “Naye aliposhuka mashuani, akaona mkutano mkuu, akawahurumia; kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji; akaanza kuwafundisha mambo mengi”

TAFAKARI: Neno liko wazi linasema Yesu aliwahurumia wale makutano. Wale watu walio kuwepo kwenye mkutano walikuwa na matatizo mengi ambapo kwa hali ya kawaida hata wangefanya matangazo ama kampeni zozote matatizo hayo yasingekwisha kuelezewa. Hata sasa tunaonyeshwa kwamba huruma yake ni muhimu sana na inapita vitu vyote, zaidi ya yote yeye atakuwa pamoja nasi popote tutakapoenda.

SALA: Bwana, kwa huruma yako tunaomba utusaidie kama ulivyowasaidia wale makutano uliowaona. Tufundishe neno lako na mambo mengi tusiyoyajua kwa maana hakuna mchungaji wa pekee kama wewe. Tunaomba hayo kwa jina lako takatifu, Amen.

 

No comments:

Post a Comment