Monday, March 11, 2013

Neno la leo

Yoh 13: 36 “Simon Petro akamwambia, Bwana, unakwendapi? Yesu akamjibu, niendako huwezi kunifuata sasa; lakini utanifuata baadaye”

TAFAKARI: Yesu ana ratiba na ajenda yake juu yetu sisi kama tutamfuata yeye na zaidi ya yote anajua akili ya kila mmoja wetu zaidi ya tujitambuavyo wenyewe. Kwa mantiki hii katika somo hili Peter hakujijua lakini Yesu alimjua kwa undani zaidi. Pengine unasita sita kumfuata Yesu sasa, kumbuka yeye anakujua zaidi na ipo siku utamfuata yeye.
SALA: Mwenyezi Mungu, tunaomba utusaidie tujitambue wenyewe na zaidi kufahamu mipango yako juu yetu na ahadi zako kwetu sisi. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment