Tuesday, March 12, 2013

Neno la leo

Yoh 21:19 “Akasema neno hilo kwa kuonyesha ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu, Naye akiisha kusema hayo akamwambia, Nifuate”

TAFAKARI: Hata baada ya kutwaliwa kwa Bwana Yesu, tumesikia hili neno nifuate ili kuepukana na mabaya mengi. Matendo na njia zetu za kumfuata Yesu Kristo ni mojawapo ya njia za maisha hususan maisha mapya ambayo hutuongoza kule apendako yeye tuelekee.
SALA: Bwana Mungu, tunaomba utuweke karibu nawe, hasa pale tunapokufuata kwa matumaini ya ufufuo wako. Katika jina la Yesu tunaomba na kuamini, Amen.

No comments:

Post a Comment