Wednesday, March 13, 2013

Neno la leo

Mt 24:4 “Yesu akajibu akawaambia, angalieni mtu asiwadanganye”

TAFAKARI: Maandiko yanaonyesha Yesu anapatwa na wasiwasi juu ya wanafunzi wake kuhusiana na habari watakazosikia na kuingia katika majaribu ya kufuata viongozi wabaya. Aliwaonya kuhusiana na manabii wa uongo, roho wachafu na matapeli waliodhani wanaweza kuendesha maisha ya baadae.
SALA: Mwenyezi Mungu tunakuomba, utufanye tusiongozwe pabaya, badala yake utupe muongozo wa kuenenda katika njia nzuri. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment