Saturday, October 27, 2012

VIFUNGO VYA LAANA


Neno LAANA katika kamusi limetafsiriwa kama ukosefu wa radhi za mwenyezi Mungu, hasira ya Mungu. Au ni apizo atoalo mtu kwa mtu mwingine ili afikwe na ubaya, uovu, msiba au hasira ya Mungu. LAANI  limetafsiliwa kama, shtakia kwa Mungu, au ombea uovu.

Zipo laana nyingi lakini leo ningependa kuzungumzia laana zifuatazo:-

  1. Ukoo/familia:- laana zinazojiendeleza kwenye ukoo hutokana na matokeo ama matunda ya dhambi. Kwa mfano unakuta katika familia husika kuna wengine wana laana za magonjwa sugu kama kansa, kwenye hiyo hiyo familia wengine hawaolewi, wengine wameolewa lakini ndoa hazidumu, wengine hawapati mimba. Familia nyingine utakuta kuna vifo vya ghafla, wanaanza maisha na kufanikiwa na kuwa na mali na biashara kubwa au kazi lakini mwisho wao wanaishia kufilisika na kufa kwa mateso makali.Unatakiwa kuomba maombi ya rehema na toba na lazima utamke kilichofanyika na matokeo yake.  Kwa sababu kila dhambi iliyofanyika ni kutokana na kuwa na miungu mingine. Dhambi inatokea pale mtu anapomwacha Mungu wa kweli na kusikiliza miungu mingine. Sasa unapokosa msaada wa Mungu wa kweli unapata misaada ya miungu inayokusababisha wewe kutenda kinyume na Mungu. “Usiwe na miungu mingine ila Mimi- Kumbukumbu la torati 5:7”
  2. Laana za kulaaniwa na mtu mwingine:- Yawezekana ulikosana na rafiki yako ama mtu mwingine pengine mwalimu wako wa shule akakuchukia na kukulaani. Anaweza kukulaani kuwa na kamwe hutakaa uendelee kwa kila utakalofanya usifanikiwe.
  3. Laana za kujilaani mwenyewe:- Kuna watu hawaridhiki na jinsi walivyo ama niseme viungo vya miili yao, yaani kwa ufupi hawajikubali ama kujiamini. Utakuta mtu analalamika na kusema “aah mimi kwa ufupi huu sidhani kama nitakaa nipate mwanamke mrefu atakaenipenda, ama mwingine atajilaani kwa kusema kamwe hawezi kuwa mtu wa kwanza darasani kwa sababu tu ya mtu fulani nyumbani kwao hajawahi kuwa” Siku zote maneno huumba na kujiumba, kwa maana hiyo yale uyatamkayo mdomoni kwako vivyo hivyo yanafanyika.
  4. Laana ya vitu visivyoisha: Kuna watu wamelaaniwa kwa kila wakigusacho kisiendelee na matokeo yake hujikuta wameanzisha vitu mbali mbali bila hata kimojawapo kukamilika. Mfano mtu anataka kujenga lakini anaishia nusu na kuanza kitu kingine ambacho nacho hakifiki mbali. Nataka kuanzisha biashara ya nguo, atanunua sehemu ya kuuzia nguo lakini hakuna kitakachoendelea. Watu kama hawa ni wale wanaonena kwa midomo lakini hawatekelezi.
  5.  Laana ya kufanya tendo la ndoa na dada yako au kaka yako, baba yako au mama yako
    Kuna mambo mengine sio rahisi hata kuelezea lakini yapo na yanafanyika mtu amelala na Dada yake, mwingine na kaka yake, laana ya Mungu imeagizwa juu
    yao “Kumb 27:22 Na alaaniwe alalaye na umbu lake, binti ya babaye au Binti ya mamae. Na watu wote waseme Amina”

Haya yote yanatokana na UPOFU wa mawazo. Akili ikifungwa mtu hawezi kufanya maamuzi yoyote. Pia akili ikifungwa mtu haoni ugumu wa dhambi. “2Wakorintho 3:14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi wakati lisomwapo Agano la kale, utaji uo huo wakaa, yaani haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo”. Soma pia Waefeso 4:18

NAVUNJAJE VIFUNGO?
Biblia inapozungumza habari ya watu waliofungwa wapate kufunguliwa, hii ina maana ya kuwa kuna watu wamefungwa chini ya utawala wa nguvu za giza katika ulimwengu wa Roho. Watu hawa wamefungwa kwenye magereza na Ibilisi.
Tutambue ya kuwa Yesu aliposema amekuja kutuokoa hii inamaanisha kwamba kuna mahali ambako tusingeweza kujikwamua wenyewe bila nguvu yake yeye mwenywe kuingia kati yetu.
Aliyahidhirisha haya kwenye kitabu cha nabii Isaya 61:1-2 Roho ya Bwana Mungu i juu yangu kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema, amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao”.
Vunja uhusiano wako na hiyo miungu pamoja na kazi zake na agano lililofanyika kati ya familia au ukoo wako na hiyo miungu. Kila unapotamka mwisho wake sema kwa sababu nimesamehewa. Ipo mistari mingi ya kuvunja maagano lakini mimi nitakupa kifungu hiki cha mstari katika kuvunja maagano na mapoozo ya aina yoyote. “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya kutiwa mafuta” Isaya 10:27
Kifungu kingine ambacho waweza tumia ni kwa kutaja maneno haya wakati wa kuvunja vifungo ama laana “Bwana Yesu, nasimama mbele zako na katika ulimwengu wa roho, kujiachanisha nafsi yangu (Taja jina lako) na vifungo vya kuzimu kwa upande wa baba yangu na mama yangu kwa sababu nimesamehewa.” Endelea vivyo hivyo kwa kutaja, roho na mwili kwa kutumia maneno hayo hayo uponyaji hufanyika katika nafsi, mwili na roho.
Mtegemee Roho Mtakatifu kwa maana atakufundisha mengi ikiwemo kuomba na maagizo ya Yesu. Na kwa kufuata maagizo ya Yesu na kuenenda kwa roho hivyo vifungo vya nafsi vitakwisha. Soma Wagalatia 5:16-25, Luka 22:40-46. Kudumu katika maombi, kuenenda kiroho na kuepuka uovu ni muhimu kwa sababu kwa kufuata misingi hiyo ndipo unafunguliwa vifungo kwa kuombewa ama kwa nguvu inayotenda kazi ndani yako kupitioa roho mtakatifu. Lakini pia ni muhimu kujua ya kwamba sala ya toba pekee haitoshi kumfungua mtu kama ana vifungo na sio imani tu bali na juhudi binafsi ya mtu itasaidia katika kumuweka huru. Wapo watu wanaotaka kupokea miujiza bila ya kuwa na mabadiliko yoyote, ama bila kusoma neno la Mungu na kukua kiroho ama bila kuomba. Wao husubiria siku za maombi, ama mikesha ama makongamano ya maombi ili waombewe kisha baada ya hapo hawajishughulishi katika kukua kiimani.
Kuwa hodari katika Bwana ili upate ulinzi wa Mungu. Waefeso 6:10-11 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za shetani”
Maana ya kuwa hodari katika Bwana ni kukaa kwenye maombi, kusoma na kulishika neno lake liwe ndani yako, na kutaka kumjua yeye zaidi. Sikuzote Sali kwa bidii katika kupambana na muovu shetani ndo mana tunaambiwa vaeni silaha zote za Mungu ili kuweza kupingana na hila za muovu shetani.

Mbarikiwe na Mungu!

 

Thursday, October 25, 2012

Mngoje Bwana!

"Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja wala hatakawia. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani, naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye" Waebrania 10:37-38

Wednesday, October 24, 2012

Mwaka wa Bwana uliokubaliwa!

"Roho ya Bwana Mungu i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema, amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo kuwatangazia mateka uhuru wao na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao" Isaya 61:1

Kipekee ni neno ambalo nikisoma nafarijika na kutambua kuwa Bwana wetu yupo sikuzote kutufuta machozi na ni tumaini la wengi waliokata tamaa. Neno hili linasema kwamba wote waliao watafarijika na kupewa taji la maua, mafuta ya furaha badala ya maombolezo na vazi la sifa badala ya roho nzito na vivyo hivyo wataitwa miti ya haki iliyopandwa na Bwana ili atukuzwe.
Yamkini unapitia mambo magumu pasipo wewe kuona njia, jua ya kuwa Mungu anaskia kilio chako. Pengine huu sio mwaka wako, lakini jua muda wako hauko mbali. Mwamini Mungu na kumtegemea kila siku. Muombe Mungu akuzidishie Imani yako katika kumwamini yeye kuwa ndiyo muweza wa kila kitu na anajibu maombi.

Mungu awabariki!

Tuesday, October 23, 2012

Zaburi ya Leo

Zaburi 92:1-2 "Ni neno jema kumshukuru Bwana, na kuliimba jina lako Ee uliye juu. Kutangaza rehema zako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku"

Sunday, October 21, 2012

NI NEEMA PEKEE HUTUOKOA


Matendo hayatuokoi bali neema hutuokoa. Mungu pekee ndiye atakayetuokoa na hivyo basi haina budi umkiri na kumwamini ndiyo wokovu unaingia halafu matendo yanafuata. “Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa yako mabaki waliochaguliwa kwa neema. Lakini ikiwa ni kwa neema, haiwi kwa matendo tena au hapo neema isingekuwa neema.” Warumi 11:5-6

Yakupasa kuufanyia kazi wokovu wako ili upate neema kutoka kwa Bwana Yesu. Katika maandiko matakatifu anatuasa ya kuwa tutimize wokovu wetu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. “Basi, wapendwa wangu kama vile mlivyotii sikuzote si wakati mimi nilipokuwa tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka” Wafilipi 2:12

Katika kufanya yote haya yakupasa kumfuata Yesu na kuwa mwanafunzi wake.Je sifa zipi zinamuonyesha mtu kuwa mwanafunzi wake? Yakupasa kutoa maisha yako na kumtumikia Yesu, Lazima uwe mfuasi wake yaani unaenda pale Yesu anataka uende, unafanya yale ambayo yeye anataka ufanye na sifa nyingine ni kujifunza zaidi kufanana na yeye. Unahitaji kuubeba msalaba katika hatua za kutaka kufanana na Yesu.

Hatua za kubeba Msalaba/ Bearing a cross

·        Jikubali (Accept who you are and don’t live in denial)-  Kama hujajikubali ulivyo huwezi kufunction vile ambavyo unafikiri ungefunction. Usijaribu kuwa mtu fulani, jikubali ulivyo. Kwa maana tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. “Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa, nimekuweka kuwa nabii wa mataifa”Yeremia 1:5

Kuna watu huwa wanasumbuliwa na vitu vidogo sana katika maisha yao. Unaweza kuta mtu hana raha analalamika yani Mungu sijui kwa nini kaniumba hivi? Ukimuuliza tatizo ni nini anaweza kukujibu kuwa sijui kwa nini mimi mweusi sana, mimi nina tako kubwa ama sina matako kabisa au sina nywele, mwingine atakulalamikia ana matiti makubwa ama hana kabisa. Ukiangalia wenzetu huku nchi zilizoendelea wanafanya vituko kweli. Kutwa kwenda kwa madaktari kuongeza/kupunguza matiti, kuchoma sindano za midomo iwe mikubwa na Kubadili jinsia na mambo mengine kama hayo. Na siku zote mwanadamu haridhiki na chochote kwa sababu wengine baada ya kufanya vitu kama hivyo nilivyotaja hapo juu bado wataona kuna kasoro nyingine na hivyo watataka kubadilisha sehemu za miili yao tena na tena. Mshukuru Mungu kwa jinsi ya alivyokuumba kwa sababu katika macho yake hakuna mtu aliye mbaya kwake. “ Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu. Na nafsi yangu yajua sana” Zaburi 139:14

·        Eneo lako ni lipi?- Lazima kukubali jaribu lako na kulifanyia kazi- Pengine jaribu lako ni kukosa mtoto ama kazi, kukosa mchumba. Yakupasa kulifanyia kazi na kumuomba Mungu akuondolee ile tabia ya kulalamika zaidi akupe maarifa ya kulifanyia kazi jaribu lako. Kamwe usijilinganishe na mtu kwamba kwa nini huyu ana hiki na mimi sina, kwa nini yeye amepata mapema nami sijapata ili hali nimeomba muda mrefu na vitu kama hivyo. Mungu hana upendeleo na mawazo anayotuwazia ni mema. Ukiendelea kuwa muaminifu kwake atakupenda daima. Jua muujiza wako uko mlangoni kwako Mungu anakusubiria ufungue mlango na uupokee. Hivyo basi ni vyema sikuzote kujiweka mtu mwenye furaha na amani ndani ya moyo wako. Mara nyingi tunalalamika pasipo kujua kwamba tunajiondolea baraka zetu wenyewe. Lijue jaribu lako na fanya kazi ya kuliombea bila kutia moyo wa mashaka.

·        Kubali jaribu lako unalopitia kwa wakati sijui kama Kiswahili imekaa sawa lakini kwa lugha ingine ni Embrace the walk- He never promised that the walk will be easy. Hakusema kila kitu kitakuwa mteremko bali ni kujibiidisha katika kumtumikia yeye. Siku zote mtu akiomba kuna majibu matatu (1) HAPANA (2) NDIYO lakini SUBIRI (3) NDIYO WAKATI NI SASA. Vita ni vingi sana hasa katika kumtafuta Mungu. Mpaka uuone mkono wake lazima kuna kupitia dhoruba nyingi. Kila jaribu linalokujia Mungu atakuonyesha mlango wa kutokea. Do not blame your past just make the most of it. Chochote ulichopitia nyuma usikilalamikie kwa sababu huo ni mtaji wako, it’s your unique story. Likumbatie jaribu lako lililokupata na kulifanyia kazi. Mfano mzuri ni Oprah, she was abused and she used that to tell stories. Ndo mana nasema that was her profit and she made the most out of it, look where she is now. Jaribu upitalo is not to break you but to make you. Tena Mungu hapendi watu wanaolalamika yaani wao siku zote kwao ni mbaya ama mambo yao hayaendi kama wanavyotaka.

Ndo mana wazungu wanasema “When the going gets tough, the tough gets going”. Kabla hujafikia malengo unayotaka kufikia lazima upitie misuko suko mingi ambayo hiyo ndiyo inakujenga. You are building muscles of your life, acha kulalamika na mtumikie Mungu.

Mungu awabariki!