Saturday, November 3, 2012

UMUHIMU WA KUWA NA MAONO


Kwanza kabisa nianze kwa kutoa maana ya maono ni fikra za kinjozi ama mtu mwenye uwezo wa kuona mbali. Ama ni ile hali ya kitu au tukio lionekanalo kwenye akili lakini kiuhalisia halipo. Kwa lugha ya kizungu naweza kusema a Vision is an experience in which a personage, thing or event appears vividly to the mind although not actually present, often under the influence of a divine or other agency. Simply it is a picture you have in mind that is going to happen.
Ni muhimu kuwa na maono kwa maana maono husaidia mtu ajue anachotaka kufanya na kwa wakati gani. Vile vile ni muhimu kwa sababu maono hutoa taarifa katika maisha ya kila siku ya mwanadamu ni jinsi gani anaweza kuepuka na jambo lolote ama atafanikiwaje kuhusiana na maono yake.
“Pasipo maono watu huacha kujizuia, bali ana heri mtu Yule ashikaye sheria” Mithali 29:18
Maono yako lazima yawe clear tofauti na ndoto. “Wasiuone mwili wake wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosemakwamba yu hai” Luka 24:23. Maono ni yale yanayotabiri mambo yatakayotokea baadae tofauti na ndoto. Mara nyingi ndoto ni accumulation ya mawazo mtu awazayo kwa siku na akilala akaota mambo yafananayo na hayo. Kwa kufanya hivyo hayo si maono, kwa sababu maono yanaweza kutokea wakati wowote iwe mchana ama usingizini.  
Ukiangalia katika kitabu cha Waamuzi mlango wa kumi na tatu pale Malaika wa Bwana alivyomtokea Yule mwanamke tasa na kumwambia atachukua mimba na atamzaa mtoto mwanamume. Ni moja ya mfano wa maono ambayo yako wazi kabisa tofauti na ndoto. “Kwani tazama utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume na wembe usipite juu ya kichwa chake maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni, naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya wafilisti” Waamuzi 13:5
Lakini vile vile ndoto zinaweza kuwa maono mfano mtu anaweza ota anapandishwa cheo lakini wafanyakazi wengine wanapinga jambo hilo na kutaka afukuzwe kazi. Maana ya ndoto kama hiyo jua ya kuwa kuna jambo zuri litatokea katika sehemu yako ya kazi lakini kutakuwa na vipingamizi. Yakupasa kuliombea jambo hilo na kukataa roho hizo za chuki juu ya mafanikio yako.
“Bwana akanijibu akasema, Iandike njozi uifanye wazi sana katika vibao ili aisomaye apate kuisoma kwa maji. Maana njozi hii bado ni wakati ulioamriwa inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake wala haitasema uongo, ijapokawia ingojee kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia” Habakuki 2:2-3

AINA ZA MAONO
·        Personal Vision: Lazima ujue nini unataka katika maisha.Kwa mfano unataka mahusiano yako yaweje iwe umeolewa ama la. What kind of legacy you want your marriage to leave behind? Kwa haraka haraka jiulize mwenyewe nini maono yako kuhusu kipato chako? Pengine unataka uwe mfanyabiashara maarufu ama mkandarasi na hujui jinsi tu ya kufikia malengo yako hayo ya kuwa mfanyabiashara maarufu. Wapo marafiki watakudiscourage kwa kila utakachofanya kwa ajili ya maendeleo yako. Na kama unataka kuendelea never fear about what others will talk about you. Na kama mpaka sasa hujui your personal vision you better find out soon as time is not on your side. Ni muhimu kujua Mungu anataka uwe nani katika maisha yako.

·        Maono ya familia/Family vision: Kwa mfano wewe umeoa/olewa, sasa mkiwa kama mke na mume yaani familia moja ni nini vipaumbele vyenu kwa maisha mapya mliyonayo? Katika tamaduni zetu za kiafrika familia ni muhimu sana. Na kwetu extended families zinapewa umuhimu na hata mara nyingine zinazidi familia za karibu yaani baba, mama, watoto. Na kama mtu utakuwa hujajua jinsi gani ya kuendesha maisha yako kama mtu na mume utajikuta hakuna maendeleo kwa sababu vipaumbele vyako vitakuwa juu ya watu wengine ama nisema ndugu instead of your immediate family.Mfano kuishi nchi za ugenini mathalan US kumefanya sense ya family kupotea na kuanza kuwa individualism. Yaani a family entails Baba, Mama na watoto. Ndugu wengine wanasahaulika huko majumbani na ndiyo maana watu wengine hupata lawama huyu ndugu yetu kabadilika sana hata hasaidii ndugu zake walioko TZ na mambo kama hayo.

Lakini tutambue kwamba Biblia inasema mtu atamuacha Baba na Mama yake ataambatana na mkewe. We should not make our descions basing on what our parents want. Hii haimaanishi kuwa uwadharau unaweza endelea kuwatafuta kwa ushauri lakini jua ya kwamba your immediate family ni mke na watoto wako. Lakini pia hii isiwe sababu ya kukuzuia kusaidia ndugu.

·        Ministry vision:- Unamfanyia nini Mungu? Lazima ujue maono yako katika kumfanyia kazi Mungu. Pengine wewe maono yako ni Mchungaji, ama sister. Ama maono yako wewe ni kusaidia maskini kama Kornelio alivyokuwa anatoa sadaka kwa maskini (soma zaidi Matendo ya mitume 10:9-30). Pia soma Waamuzi 13:2-24 na pia Kitabu cha Daniel kwa ufunuo zaidi juu ya maono.
Mungu awabariki!

Thursday, November 1, 2012

SIKU YA WATAKATIFU

Leo ni sikukuu ya Watakatifu wote. Tunaitumia siku hii kuwakumbuka wapendwa wetu waliotwaliwa na Mwenyezi Mungu. Kipekee namkumbuka Mama yangu mpendwa Mariam Jambia na my little brother Adam. There are times I just wish you are here by my side. I have so many things to share with you Mum. Thank you for shaping me into a person who I like and proud to be. Let me tell you something, you know I'm now married to a wonderful husband most women would wish to have. He is a great person and I thank God for having him. I'm sure if you have had a chance to meet him you would have agreed with all kind of praises about him. On that same day of our wedding, I looked up to see if you can give me a hand in applying my last last make-up before entering the Church. I remember you whispered into my ears, "Kisura wangu I'm not good in make-ups, you know how natural I am". Let me just fix your hair. I felt your hand in my hair and that is when I knew you were besides me all along. Words cannot express how much I miss you dear Mother. You were the greatest thing could have ever happened to me. Not a day goes by without thinking about you especially now when I want to enjoy this good life with you. But I thank God for everything, and I'm proud to be called the daughter of Mariam Jambia. May the almighty God continue to rest your souls in eternal peace.
Also nawakumbuka wakwe zangu Mr & Mrs Willness Lyimo. Always mnakumbukwa na watoto wenu (Jackson, Anitha, Linda, Steve & Manny), wakwe zenu (Dennis, John and Myself), wajukuu (Brianna Lyimo, Austin Adhero, Isaac & Aaron William Rweikiza), ndugu, majirani na marafiki zenu.
My late sis in law Glory Lyimo you were one of a kind. I remember when you were in your A-level studies at Kibosho girls secondary school, I used to admire you so much and your friends sis Maria, Nelly, Chegy and many more. You were full of fun. How ironic life can be, who would have thought I will become one of the members in your family? We live in such a small world, look at me now I'm  called Mrs Jackson Lyimo.
We always pray for you guys and that our living God continue to rest your souls in peace. We love you all and forever will be in our thoughts.
Tunawaombea pia Ndugu, jamaa na marafiki zetu wengine waliotwaliwa na Mungu wapumzike kwa Amani.
Amen!

Tuesday, October 30, 2012

Natembea na Mungu

"Basi jueni ya kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao na kushika amri zake, hata vizazi elfu." Kum 7:9

Monday, October 29, 2012

Zaburi ya leo

Zaburi 35: 4-5  "Waaibishwe, wafedheheshwe wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma wafadhaishwe wanaonizulia mabaya. Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa Bwana akiwaangusha chini"