Friday, March 15, 2013

Neno la leo

Mt 15:14 “Waacheni hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimuongoza mwenzake watatumbukia shimoni wote wawili.

TAFAKARI: Katika maisha ya kawaida tunahitaji vingozi wanao ona. Kiongozi asiyeona vizuri bila shaka huyo ataleta matatizo. Kama tukiwa wenye busara, tunamfuata Kristo kwa sababu yeye huona vizuri zaidi. Na kwa ajili yake wale wenye kuona anawapa sababu ya kwamba yeye ndiye kiongozi mkuu na hakuna wa kufanana nae.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba tusiwe vipofu wa upofu wa wale wanaotuongoza isivyo. Tunaomba kwa ajili ya kuona na usalama katika maisha yetu. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment