Thursday, March 14, 2013

Neno la leo

Mt 17: 1 “Na baada ya siku sita, Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo na Yohana nduguye, akawaleta juu yam lima mrefu faraghani”

TAFAKARI: Baadhi ya hadithi za Yesu zinaonyesha ukweli wa mambo yajayo. Kila mara tunaposali, tunaposoma neno la Mungu, ama kutafakari juu ya Imani aliyotupa, tunapata sababu ya kumwamini hasa pale anapotuamuru kumfuata yeye.
SALA: Mungu wetu na Baba yetu, tunataka utuongoze juu ya kilele cha mlima ili tupate uzoefu mkubwa wa kutambua sauti yako utuitapo na kuweza kubadili maisha yetu. Katika jina la Yesu tunaomba na kuamini, Amen.

 

No comments:

Post a Comment