Friday, March 8, 2013

Neno la leo

Yoh 12:26 “Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo”

TAFAKARI: Leo tuna nafasi iliyotolewa na Yesu kwa wanafunzi wake, yaani hatuwezi kumtumikia bila kusimama imara na kufuata maelekezo yatolewayo na neno lake. Ameahidi kuwepo popote pale tutakapokuwapo, kwa hiyo hakuna budi kumtumikia yeye.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba tusikie uwepo wa ahadi yako ya kuwepo nasi pale shughuli tuzifanyazo za kukutumikia wewe zitatupeleka. Usikae mbali nasi Bwana kwa maana tunahitaji muongozo wako pale tutakapokwama. Ni katika jina lako takatifu tunaomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment