Monday, March 4, 2013

Neno la leo

Yoh 8: 12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”

TAFAKARI: Katika maisha ya kawaida wengi wetu tunaogopa giza, hii inatokana na kwamba tumekuwa tukiambiwa kwamba mambo mabaya mengi hufanyika gizani. Basi kwa hofu hiyo hiyo tuache mambo ambayo yanatuweka gizani na tumfuate Yesu, yeye awe taa itumulikiayo usiku na mchana.
SALA: Mwenyezi Mungu tunaomba utumulike katika maisha yetu, ili tunapokufuata katika njia yako tusiteleze na kuanguka chini. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment