Tuesday, March 5, 2013

Neno la leo

Luka 7:9 “Yesu aliposikia hayo alimstaajabia, akaugeukia mkutano uliokuwa ukimfuata akasema, nawaambia, hata katika Israel sijaona imani kubwa namna hii.

TAFAKARI: Kuna wakati watu wanakua wadadisi juu ya kwamba wakae na makundi gani pindi wakiwa wamempokea Yesu na kumfuata yeye. Huangalia kwamba huyu mtu ana imani gani juu ya Mungu ambapo anaweza kuwa mfano kwa wengine. Lakini Yesu, anasema tusibague watu na tuwe wakarimu kwa watu tusiowajua, tuwapende wale wenye mapungufu na tofauti nyingi, kufungua milango kwa wageni. Tuzidishe Imani yetu kwa yeye kwa sababu ndiye mponya wa pekee.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba usikie vilio vyetu pale tukuitapo. Tujaze mioyo yetu kwa Imani kuu inayoshangaza na kuponya wengi. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment