Wednesday, March 6, 2013

Neno la leo

Luka 9:61 “Mtu mwingine pia akamwambia, Bwana nitakufuata; lakini nipe ruhusa kwanza nikawaage watu wa nyumbani kwangu”

TAFAKARI: Tunapoweka ahadi ya kumfuata Yesu, lazima tukumbuke kwamba hakuna kugeuka nyuma. Ukijitoa kwake basi fanya kazi zake kwa kutimiza mapenzi yake. Lakini endapo tutakuwa tumejitoa kwa kazi nyingi basi kuna wakati tutapata sababu za kujiengua kuwa karibu naye.
SALA: Mwenyezi Mungu, tupe busara na maarifa ya kutenga vipaumbele vyetu katika misingi iliyo sahihi na zaidi tupe nguvu ya kufanya maamuzi yetu kwa hekima. Tunaomba hayo kupitia mwana wako na Bwana wetu Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment