Thursday, March 7, 2013

Neno la leo

Yoh 10: 4 “Naye awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake”

TAFAKARI: Kama wanadamu tunafahamu kondoo walivyo, hivyo basi tujiweke kwenye huu mfano wa kondoo wanaochungwa. Kwa mfano kondoo wengine ni wale wasio na muelekeo, wengine wanatembea taratibu sana na hata hulazimika kuchapwa ndiyo wapige hatua. Na wale wanaosikia sauti ya mchungaji akiamuru na hupiga hatua kufuatana na hiyo. Tujue kwamba, kusikia na kutambua sauti si tatizo, bali cha muhimu ni kumfuata mchungaji.
SALA: Bwana Yesu tunaomba utuongoze tusikie sauti yako na kukufuata wewe kwa sababu tunafahamu wewe utatulinda na kutulisha chakula kilicho kamili. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment