Friday, March 1, 2013

Neno la leo

Mt 7:17 “Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri na mti mwovu huzaa matunda mabaya”

TAFAKARI: Neno liko wazi kabisa, kwamba hakuna mti ambao umestawi kwa kuwekewa mbolea nzuri ukazaa matunda mabaya. Na vivyo hivyo, mzabibu hauwezi kuzaa miiba, ama mchungwa kuzaa maembe. Muombe Mungu akusaidie utende mema na uzidi kumtegemea yeye. 
SALA: Mwenyezi Mungu, Asante kwa kutukomboa kwa damu ya mwana wako Yesu Kristo, Bwana tunaomba uzidi kutunyunyizia mbolea yako ya Imani ili tukastawi na kukua zaidi kiroho, kamwe tusirudi nyuma. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment