Wednesday, February 27, 2013

Neno la leo

Rum 8: 14 “Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu”

TAFAKARI: Wakati wa kwaresma ni muda ambao tunakuwa wenye kusafishwa na roho wa Mungu. Ni roho mtakatifu wa Mungu ndiye anaetukusanya pamoja na wote wamfuatao Kristo, ni kama kondoo waliopotea wanaporudishwa zizini hali kadhalika habari za mwana mpotevu nae alipoamua kurudi kwa baba yake. Hivi vyote havikutendeka pasipo kuongozwa na roho wa Mungu.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba roho wako mtakatifu atuongoze ili tuweze kutambua nafasi zetu katika familia na kutenda yale yanayokupendeza wewe. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment