Monday, February 25, 2013

Neno la leo

Mt 19: 21 “Yesu akamwambia, ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini nawe utakuwa na hazina mbinguni; kasha njoo unifuate”

TAFAKARI: Katika hili zawadi ya bure ya Mungu inakuja na gharama na ulazima. Ni juu ya sisi kutambua ni vitu gani tunavijali zaidi. Lakini vilevile, tunapata faida kubwa pale tujuapo mualiko wa Mungu ni wa haraka mno na kujua maisha ya kumfuata yeye ni ya utajiri mkubwa.
SALA: Bwana, tunaomba utangulize matakwa ya maskini na wahitaji wako juu yetu hasa pale tunapokuwa na nafasi ya kuchagua katika vile ulivyotupa.  Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment