Friday, February 22, 2013

Neno la leo

Mt 9:9 “Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata”

TAFAKARI: Pengine wakati ule wa kipindi cha utozwaji wa ushuru wa hali ya juu na unyanyaswaji wa watu, ulimuingia Mathayo na kuchoshwa nao. Huenda aliskia habari za Yesu aliyekuwa anahubiri habari njema kuhusu ufalme wa mbinguni, alikuwa anaponya wengi na kuwavuta karibu. Aliposkia tu sauti ya Yesu akimuita aliruka haraka na kumfuata. Je, tunajifunza nini juu ya habari hii?
SALA: Bwana tunaomba uwe mwenye uvumilivu nasi pale tunapojishauri kuitikia mualiko wako wa kukufuata.Tunaomba utuvute karibu nawe nasi tuwe miongoni mwa wafuasi wako, katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment