Wednesday, February 20, 2013

Neno la leo

Mt 8:19 “Mwandishi mmoja akamwendea, akamwambia, Mwalimu, nitakufuata kokote uendako”

TAFAKARI: Ukisoma hadithi ya mwandishi aliyeonekana katika kitabu hichi cha Mathayo kwa haraka unaweza kusema ameonyesha maana ya kumfuata Yesu na Kujitoa kwa ajili yake (to follow and then made a daring commitment). Lakini vilevile, waweza kusema kuwa alikubali kumfuata bila kujua kuna gharama yake, yaani safari ya kwenda mbinguni sio rahisi lazima mtu utakumbana na vikwazo. Mungu anahitaji watu ambao watajitoa kwake kwa moyo wote na sio kwa kusita sita na kurudi nyuma.
SALA: Mwenyezi Mungu, tunaomba utusaidie tuweze kusikia sauti yako na kuyatoa maisha yetu kwako ili tuishi kwa kukutegemea wewe daima. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment