Tuesday, February 19, 2013

Neno la leo

Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo”

TAFAKARI: Mungu ametuachia amani. Na vitu anavyotupa haviwezi kufanana na vile atoavyo mwanadamu. Yamkini ni magari ya kifahari, pesa nyingi, na vingine vifananavyo na hivyo, kamwe haviwezi kufanana na vitu atupavyo Mungu.
SALA: Mwenyezi Mungu tunakushukuru kwa upendo wako wa ajabu. Umetupa amani katika nchi zetu lakini kwa kukosa maarifa tumeshindwa kutumia ipasavyo yale unayotupa. Tusamehe Bwana na tunaomba ukalete amani na upendo miongoni mwetu. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment