Thursday, February 28, 2013

Neno la leo

Mk 2: 15 “Hata alipokuwa ameketi chakulani nyumbani mwake, watoza ushuru wengi na wenye dhambi waliketi pamoja na Yesu, na wanafunzi wake kwa maana walikuwa wengi wakimfuata”

TAFAKARI: Mara nyingi watu huchagua marafiki ambao tabia na hadhi zao zinaendana. Hii hupelekea kujitenga na wale wanaoonekana watenda dhambi na penginge kuwanyooshea vidole. Lakini katika maisha ya kumfuata Yesu hatufundishwi hivyo, bali anahimiza kuwa karibu na wenye dhambi ili tuweze kuwasaidia katika hatua zao za kubadilisha maisha yao.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba utusaidie ili tuweze kukaa pamoja na wenye dhambi wanaojitoa kukufuata wewe. Tupe busara na maarifa katika kushiriki nao kwenye shughuli mbali mbali na hata kuwapa mafundisho utoayo wewe tukiongozwa na roho mtakatifu wako. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment