Tuesday, February 26, 2013

Neno la leo

Mt 9: 27 “Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu mwana wa Daudi”

TAFAKARI: Kuna wakati mtu unaona muda huu ni mdogo hautoshi kwa Mungu kuniskia pale nitakaposali, lakini kwa imani ukipaza sauti na kuomba kwa nguvu, hatimaye maombi yako hujibiwa. Ni imani tu inapeleka mtu kupata hitaji lake toka kwa Bwana ama kupona.
SALA: Bwana Mungu, tusamehe pale ambapo tumekosa na kushindwa kukuamini wewe ya kuwa unatenda miujiza. Tusaidie tuone na kwa imani tu tuwezeshe tuone zaidi na zaidi rehema zako za ajabu. Katika jina la Yesu, tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment