Sunday, March 17, 2013

Kumtii Mungu

Mzazi anapomuagiza mtoto wake afanye jambo fulani, mara nyingi mtoto anapaswa kutekeleza agizo hilo.  Mzazi anategemea mtoto atafanya alivyoagizwa na si vinginevyo kwamba kutakuwa na mabishano ya kwa nini mtoto huyo anatumwa. Mfano huu wa mzazi ni mfano wa agizo ambali halihitaji mjadala kwa maana nyingine ni agizo kamilifu

Pia kuna amri au maagizo ambayo yanahitaji mjadala ambapo ili zitekelezeke. Kwa mfano amri/agizo zinazowekwa na serikali ni zile amri ambazo mara nyingi zinahitaji mjadala. Yaani zitakapotolewa mtu atauliza kwa nini napaswa kutii hii amri? Kisha ataelezwa matokeo ya kutii na kutotii amri hiyo.
Tukija upande wa Baba yetu mbinguni, amri zake na maagizo yake ni sawa na maagizo au amri atoazo mzazi kwa mtoto wake, yaani  hayahitaji mjadala. Kwa maana nyingine amri/ maagizo hayo ni kamilifu.

Ukisoma kitabu cha KUTOKA 20 habari yote inaelezea amri na maagizo Mungu aliyotoa ambayo ni kamilifu. Mungu wetu ametupa amri kamilifu kwamba hataki kuchanganywa na kitu chochote kwa maana yeye ni Mungu mwenye wivu.  Mstari wa 5 unasema  “Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao”
Wapendwa katika kipindi hiki cha Kwaresma, tunapotafakari kuteswa  kwa BWANA wetu Yesu Kristo, tunatakiwa kuendelea kuzitii amri zake na kufuata maagizo yake bila mjadala kwani amri zake zimekamilika na ni rahisi kuzifuata. Ni amri ambazo hazina maswali ya “KWA NINI?”

Mbarikiwe!

No comments:

Post a Comment