Tuesday, March 19, 2013

Neno la leo

Mt 9:38 “Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”

TAFAKARI: Wale wanafunzi 12 wa Yesu ndiyo mavuno ya mwanzo. Lakini Yesu aliona kwamba hawatatosheleza kwa kazi yake. Kutokana na kwamba alikuwa mwenye upendo na wengi hivyo kuona haja ya kuendelea kuwaita karibu watu wake ambao wako tayari kumfuata yeye. Yeye ametumia watu aaminio kwamba watakuwa wavunaji wa wengine na hivyo kuwaokoa. Ahadi yake inasema ombeni nanyi mtapewa basi tusikome kuomba na kuonyesha upendo juu ya wengine.
SALA: Ee Bwana wa mavuno, ulituambia tuombe, na sasa tunafanya hivyo Bwana, tukiomba uzidi kutuma wavunaji wako waje kutuokoa katika dhambi. Tunaomba na kupokea katika jina lako takatifu, Amen.

No comments:

Post a Comment