Wednesday, March 20, 2013

Neno la leo

Mk 10:32 “Nao walikuwako njiani, huku wakipanda kwenda Yerusalemu; na Yesu alikuwa akiwatangulia, wakashangaa, nao katika kufuata wakaogopa. Akawatwaa tena wale Thenashara, akaanza kuwaambia habari za mambo yatakayompata”

TAFAKARI: Ni sawa kuwa na hali ya kushangaa na tunaruhusiwa kufanya hivyo. Unaweza fikiria kwamba watu wanaomfuata Yesu hawawezi kushangazwa na kitu chochote. Lakini habari zinaeleza walishangaa na tena hata kuingiwa na uwoga. Nani ambae hatashangaa wala kuogopa akisikia Yesu alivyotabiri kifo chake na hata miongoni mwa wanafunzi wake watamkana?
SALA: Bwana Yesu, tunaomba utuongoze katika safari zetu na utuzidishie nguvu, ondoa hofu ya uwoga ndani ya mioyo yetu. Katika jina lako takatifu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment