Thursday, March 21, 2013

Neno la leo

Lk 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”

TAFAKARI: Kwaresma ni wakati ambao tunapewa maagizo kuhusiana na vitu tunavyofanya.Yesu hakuwatuma wanafunzi wake ili awatelekeze, la hasha bali aliwafanya wawe wa kwanza. Katika maisha yetu ya kawaida, tunapofanya jambo kwa wasi wasi ama kukata tamaa, tukumbuke kwamba yeye yupo pamoja nasi na ameshatangulia kufanya lile tuwazalo.
SALA: Bwana Yesu, tunaomba utuongoze kwenye njia yako, ikiwa uko mbele yetu ama uko nyuma basi tunajua ya kwamba ni kwa mapenzi yako na kwamba upo nasi siku zote. Katika jina la Yesu tunaomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment