Saturday, January 26, 2013

UHUSIANO WETU NA BABA YETU WA MBINGUNI

Labda nianze kwa kuuliza uhusiano wa mzazi na mtoto kwa maisha yetu ya kila siku ukoje? Kwa maisha ya kawaida mtoto akiamka humuomba Baba ama Mama ampe kitu chochote au amfanyie kitu chochote na mzazi huyo bila kusita atafanya.
Lakini kadri mtoto anavyokua na kuendelea kumuomba mzazi wake kitu inafikia wakati mzazi anachoka na pengine kuanza kulalamika ya kuwa mtoto huyu anaomba sana.
Vivyo hivyo ni sawa na maisha yetu na Mungu baba wa mbinguni. Naye vile vile huwa anachoka pale kila saa tunapoomba atutimizie mahitaji yetu.
Yoh 1:11-13 “Alikuja kwake wala walio wake hawakumpokea. Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu”
Anatuambia wale wote waliompokea wamefanyika kuwa watoto wake. Je unamfurahishaje baba yako wa mbinguni kama umfurahishapo mzazi wako. Waweza kusema ni kwa kufuata yale atufundishayo na kuendenda katika njia anazotuongoza yeye. Lakini kwa kumfanyia vitu ambavyo yeye atajiskia furaha ya kuwa mwanangu kafanya haya machoni pangu na imenipendeza.
Ni vyema unapoamka ukamshukuru Mungu kwa kukuamsha salama. Mwambie asante Mungu kwa kuniamsha salama nikiwa mwenye nguvu na afya tele. Muulize Mungu nikufanyie nini kwa siku ya leo? Ama nikuimbie nyimbo gani leo? Nikusomee zaburi gani Bwana? Mueleze ya kwamba unatambua vipaji vingi alivyokupa na muulize ungependa uwabarikije wengine kwa vipaji hivyo? Nina hakika kwa kufanya hivyo moyo wako utakua umejawa na furaha na siku yako itakuwa nzuri.
Hata katika maisha ya kawaida si mzazi unafurahia sana pale mtoto anapokufanyia kitu? Unafurahi kuona mtoto amekupikia, amekununulia zawadi kwa uwezo wake mwenyewe na mambo mengine yanayofanana na hayo. Hiyo ni mifano ya kufananisha na maisha ya kumtumikia Mungu wetu.

Jenga tabia hiyo ya kuamka na kumuuliza Mungu umfanyie nini badala ya kuamka na kumuomba tu kila siku akusikilize na akusaidie wewe tu. Kwa kufuata haya moyo wako utakusukuma kufanya mambo mengi kwa kuongozwa na roho mtakatifu.

Mbarikiwe!

No comments:

Post a Comment