Friday, January 25, 2013

Neno la leo

Mithali 13:2-3 “Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake; Bali nafsi ya mtu haini itakula jeuri. Yeye alindaye kinywa chake huilinda nafsi yake; Bali afunuaye midomo yake atapata uharibifu”

TAFAKARI: Maneno mema huleta thawabu, lakini matokeo ya maneno ya hila ni jeuri. Kauli yenye nidhamu ni muhimu kwa sababu maneno yenye ukali huleta uharibifu.
SALA: Mwenyezi Mungu, wewe uketiye mahali pa juu palipoinuka, asante kwa wema wako kwangu. Mungu naomba utakase kinywa changu nikapate kutamka yale yanayokupendeza.Nipe ulimi wa kunena maneno yenye busara kamwe nisiteleze na kutamka maneno yenye kuleta uharibifu. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment