Tuesday, January 22, 2013

Neno la leo

Mithali 10:6-7 “Baraka humkalia mwenye haki kichwani; bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka, bali jina la mtu mwovu litaoza”

TAFAKARI: Matendo ya mtu huonyesha tabia yake ikiwa ni mbaya au nzuri na sifa yake itaendelea kuwepo hata baada ya kufa.

SALA: Mwenyezi Mungu nakushukuru kwa upendo wako mkuu kwangu. Bwana naomba niongoze nikaishi kwa kufuata misingi yako niepukane na majaribu ya kutenda uovu. Vishawishi ni vingi katika ulimwengu wa sasa lakini naamini nikikutegemea wewe kamwe sitaanguka katika uovu. Nipe faraja ya kulitamka jina lako kila inapoitwa leo. Naomba hayo nikiamini katika jina la Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment