Thursday, January 24, 2013

Neno la leo

Mithali 10:18 “Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, na yeye asingiziaye ni mpumbavu”

TAFAKARI: Siku zote mtu mwenye chuki ndani ya moyo wake maneno yake huwa ya unafiki ama yenye kuudhi au uchochezi.
SALA:  Mwenyezi Mungu wewe uliye mwingi wa rehema, naomba usininyime rehema zako Baba, niangazie nuru ya uso wako na zaidi ukaniepushe na watu wabaya, wenye chuki na wachonganishi. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment