Sunday, January 20, 2013

Ujumbe wa Jumapili ya leo

Zab 27:3 “Jeshi lijapojipanga kupigana nami, moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, hata hapo nitatumaini”

TAFAKARI: Ukiwa unamtegemea Mungu hakuna upanga utakaosimama juu yako. Ukiwa naye ndani ya moyo wako hakuna vita yoyote itakayokushinda kwa maana yeye ni mshindi wa yote.

SALA: Mungu baba, wewe uliye jemadari wa vita naomba ukaimarike ndani ya moyo wangu nikutegemee wewe siku zote. Nataka kufanana nawe Mungu wangu kwa maana wewe  haubadiliki kama wanadamu. Mkono wako wa baraka usinipite eeh Mungu mwenye rehema nyingi. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment