Wednesday, January 23, 2013

Neno la leo

Mithali 10:8-9 “Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka. Aendaye kwa unyofu huenda salama, bali apotoshaye njia zake atajulikana”

TAFAKARI: Mtu hujenga hekima kwa njia ya kujifunza na si kwa njia ya kujisifu. Mtu mwenye kuishi maisha ya unyofu humpatia hekima na usalama na si kwa njia ya shughuli zake za hila.

SALA: Bwana nimekutumaini wewe sikuzote nisiaibike, naomba unijaze maarifa, hekima na uniondolee majivuno ndani ya moyo wangu ili nikaishi kwa kukufurahisha na kukutumikia wewe. Amen

No comments:

Post a Comment