Monday, January 28, 2013

Neno la leo

Mithali 14: 6, 8 “Mweye dharau hutafuta hekima asiipate; bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu, akili za mwenye busara ni kujua njia yake; lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu”

TAFAKARI: Mtu mwenye kufikiri kwamba anajua mambo yote kamwe hawezi kuwa na hekima ya kweli. Kwa maana hiyo hatakuwa na utambuzi mzuri kuhusu maadili mema ya maisha.

SALA: Mungu wangu naomba utakase ufahamu wangu ili niweze kutambua na kuchuja mema na mabaya. Zaidi nijaze roho wa kujishusha mbele ya macho yako na jamii inizungukayo.Naomba baraka zako ziwe nami daima. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kushukuru, Amen.

 

No comments:

Post a Comment