Wednesday, January 30, 2013

Neno la leo

1Yohana 5:14 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.

TAFAKARI: Mungu husikia pale tumuitapo na tumuombapo kitu. Ni zawadi kubwa pale unapojishusha kwa Muumbaji wetu. Hata zile nyakati ambapo mtu huona kwamba amekata tamaa akilitaja jina la Bwana hujua ya kwamba yeye anasikia.
SALA: Bwana asante kwa kuniskia. Maskio yako, yako wazi kwa moyo wangu huu mhitaji, Umenijibu maswali mengi yaliyo kichwani na moyoni mwangu, hakika nasema asante. Naja mbele zako nikitafuta tumaini lako na majibu yenye baraka. Katika jina la Yesu, naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment