Friday, February 1, 2013

Neno la leo

Zaburi 63:3 “Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; midomo yangu itakusifu”

TAFAKARI: Fadhili za Bwana ni za milele na hivyo hatuna budi kulitangaza jina lake na kumsifu yeye daima.
SALA: Kitu ninachokipenda katika maisha haya ni mifano ya uzuri wako, wewe utendaye miujiza mikuu siwezi kamwe kuwa na mashaka nawe. Naomba nikuimbie nyimbo za kukusifu na kukuinua wewe Mungu, zaidi ndimi zangu ziinue jina lako Bwana kwa maana hakuna kitu chochote kizuri kitakachoshindana na upendo wako. Katika jina la Yesu naomba na kushukuru, Amen.

No comments:

Post a Comment