Thursday, January 31, 2013

Neno la leo

Yeremia 5:23 “Lakini watu hawa wana moyo wa kuasi na ukaidi; wameasi, wamekwenda zao”

TAFAKARI: Moyo wa kuasi na wenye ukaidi humtenga mtu asiwe karibu na Mungu.
SALA: Mungu wewe uchunguzaye moyo wa kila mtu na kujua tabia zao naomba nimulike Mungu wangu kwa taa yako, nakiri kwamba natakiwa niache tabia yangu hii mbaya, ni nani wa kuniweka huru kama sio wewe Bwana wangu? Niondolee ukaidi ndani ya moyo wangu na zaidi unitenge na maovu mengi ya dunia hii.Asante Bwana kwa maana umeniweka huru. Naomba na kupokea katika jina la Yesu kristo, Amen

 

No comments:

Post a Comment