Tuesday, January 29, 2013

Neno la leo

Mithali 18:22, 24 “Apataye mke apata kitu chema; naye ajipatia kibali kwa Bwana. Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.”

TAFAKARI: Mke mwema ni rafiki bora kuliko wote na vile vile urafiki wa kweli hauvunjiki upesi wala hautofautishi tajiri na maskini.

SALA: Bwana Mungu asante kwa kunipa mke mzuri uliyemchagua wewe. Naomba ukazidi kuibariki ndoa yetu tukaishi kwa amani na furaha siku zote. Zaidi tunakuomba utupe marafiki wema na ututenge na wale marafiki wabaya. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kushukuru, Amen.

No comments:

Post a Comment