Monday, May 6, 2013

Neno la leo

Ayu 2:10 “Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya?”

TAFAKARI: Pale mambo yetu yanapoenda kama tulivyopanga hususan kwenye kazi zetu, familia zetu na hata kiroho tunakubali ya kwamba Mungu wetu hajatuacha. Lakini pindi tukipatwa na matatizo basi tunaanza kushuku uwepo wa Mungu na kulalamika kwamba ametuacha.
SALA: BWANA, natambua ya kwamba wewe si Mungu mwenye upendeleo, na huwezi kunipa jaribu nitakaloshindwa kulibeba. Nisaidie niweze kutambua zaidi uwepo wako kwangu, nifundishe rehema zako ili nisiweze kujiuliza mara mbili mbili kuhusu rehema hizo. Zaidi naomba nione kila jaribu nipitalo kama fursa ya kukubali yale yote uliyoniandalia. Naomba na kupokea katika jina la Yesu, Amen.

No comments:

Post a Comment