Tuesday, May 7, 2013

Neno la leo

Rum 13:8 “Msiwiwe na mtu chochote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria”

TAFAKARI: Upendo ni tunda pekee Mungu alilotuachia. Hatuna budi kupendana kwani kinyume na kuhakikisha wale tuwapendao wako karibu na Mungu.
SALA: Mwenyezi Mungu, naomba Ufunuo wa mahusiano mapya na familia yangu na marafiki zangu. Moyo wangu umejawa na mambo mengi hata mara nyingine nasahau upekee wa kila uhusiano nilio nao kati ya jamaa zangu. Nakushukuru kwa ajili ya watu ulionipa wanaoniletea furaha, wanaoniombea, wanaonifariji na ambao ni mfano wa upendo wako. Naomba uzidi kuimarisha mahusiano yangu na watu hawa ili tudumu katika pendo daima. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment