Wednesday, May 8, 2013

Neno la Leo

Yak 3:17 “Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki”

TAFAKARI: Mtu mwenye hekima huonekana machoni pa watu. Vivyo, hivyo mtu mwenye fitina, mnafiki huonekana wazi pia. Inatupasa kuomba hekima toka kwa Mungu ili tuweze kuishi vyema na jamaa zetu na zaidi ya yote turithi ufalme wa mbinguni.
SALA: Mwenyezi Mungu, wewe uliyesema hekima itokayo kwako ni ya Amani na ni safi yenye upole, naomba nizidishie hekima hiyo ili niweze kushinda hila za mwovu shetani.Nakuomba unimiminie mafuta yako ya baraka uondoe chembe chembe yoyote ya kiburi, unafiki na fitina ndani ya moyo wangu. Nifanye niwe wako Bwana, katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment