Thursday, May 9, 2013

Neno la leo

Zab 89:34 “Mimi sitalisahau agano langu, Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu”

TAFAKARI: Yote Mungu aliyoyaahidi kwako yatatimia. Yeye ni mwaminifu wa ahadi zake, hivyo unapoamka asubuhi ya leo neno hili likutie nguvu na kukupa ujasiri wa kumwambia shetani leo ni mwisho wa uongo wake katika maisha yako.
SALA: Mwenyezi Mungu nasema asante kwa kunipa nguvu na ujasiri wa kushinda mipango ya ibilisi shetani. Nakataa roho za kukata tamaa na kushindwa, nakataa roho za kiburi, fitina na majivuno. Asante Bwana kwa maana nimeona ahadi zako zikitimia kwangu. Nakushukuru Bwana kwa maana hujaniacha na unisamehe pale ambapo niligeuza uso wangu mbali na macho yako. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment