Friday, May 3, 2013

Neno la leo

Gal 6:10 “Kwa hiyo kadri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio”

TAFAKARI: Kusaidia jamaa ni kitu muhimu sana. Na Mungu ametusaidia kuona katika uzoefu wa maisha yetu ukarimu wa kitu kidogo unavyokuwa muhimu hasa kwa mtu aliyetendewa vyema. Hii inatusaidia kujenga mahusiano mema na watu watuzungukao.
SALA: Bwana naomba niongoze katika kutenda hasa mambo mema. Niongoze kwa watu unaotaka mimi niwatumikie na kuwasaidia na zaidi tengeneza nia safi ndani ya moyo wangu ili niweze kufanya mema kwa ajili ya utukufu wako na si kwa ajili ya kujivunia mwenyewe. Nisaidie niweze kufikia na kuanzisha mahusiano ya kweli na jamaa zangu, nikikutegemea wewe tu. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

 

No comments:

Post a Comment