Thursday, May 2, 2013

Neno la leo

Zab 25:4-5 “Ee BWANA, unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako, Uniongoze katika kweli yako, na kunifundisha. Maana wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, nakungoja wewe mchana kutwa”

TAFAKARI: Yatupasa kuondoa upofu wetu kimwili na kiroho ili tuweze kuona uzuri wa ngome ngome aliyotujengea Mungu wetu.
SALA: Baba wa mbinguni, wewe uonae yote yanaoyoendelea katika maisha yangu, nafurahi kwa kutambua hili kwa maana napata amani nikikufikiria wewe katika kila hatua ya maisha ninayopiga. Bado nina shauku la kuendelea kujua nini umeniandalia katika maisha yangu ya baadae, na hivyo naendelea kujitoa kwako unitumie upendavyo.  Naomba hayo na kupokea, katika jina la Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment