Monday, April 29, 2013

Neno la leo

Zab 119:90 “Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa”

TAFAKARI: Mungu aliumba ulimwengu na viumbe vyote ambapo kila kiumbe kilikuwa na madhumuni ya uumbaji wake.
SALA: Mwenyezi Mungu, naomba niweze kuendelea kubeba hadithi za utakatifu wako na kusimulia wengine. Uumbaji wako umetukuka na hakika wewe ni mfalme wa wafalme. Naapa kukutukuza wewe mimi na familia yangu kwa maana uzuri wako hauna kipimo kabisa. Naomba BWANA unifanye niwe mtoto wako mwaminifu hata mpaka ukamilifu wa dahali. Naomba hayo yote na kupokea kupitia mwanao wa pekee, Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment