Friday, April 26, 2013

Neno la leo

Kol 4:2 “Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani”

TAFAKARI: Yatupasa kumuomba Mungu kwa bidii zote ili atufungulie milango ya baraka na kueneza siri ya neno lake la uponyaji. Tumuombe zaidi Mungu atupe shauku la kutaka kusali.
SALA: BWANA, nataka kuona na kutambua kazi yako katika maisha yangu. Yaongoze macho yangu katika kuona pale unaposikia na kujibu sala zangu. Na zaidi nipate kukujua wewe vizuri kila siku ninapokutana na wewe. Naomba unijaze kwa maarifa yako na akili zako Ee BWANA, nipe nguvu nisimame imara katika kujitoa kwangu, kwako. Naomba hayo yote katika jina la Manao Yesu Kristo ashiye na kutawala daima milele.

No comments:

Post a Comment