Tuesday, April 23, 2013

Neno la leo

Mt 6:3-4 “Amin, nawaambieni, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume. Sadaka yao iwe kwa siri; na baba yako aonaye sirini atakujazi”

TAFAKARI: Ni vigumu kwa mtu kutoa msaada na asitake julikana ya kwamba amesaidia. Watu wengi wakitoa misaada mbalimbali hupenda kuhusisha vyombo vya habari ili wajulikane ya kwamba wanasaidia. Lakini tunasahau kwamba Mungu anaona mioyo yetu na hupendezwa na utoaji wetu.
SALA: Bwana Mungu, niwezeshe nione kwamba kila ninapotoa sadaka, misaada yangu na wakati wangu iwe ni kwa utukufu wako. Kwa maana napata vyote toka kwako hivyo sifa na utukufu nakurudishia wewe. Nipe roho ya unyenyekevu ili kwamba baraka za utoaji zikae ndani ya moyo wangu. Naomba na kupokea katika jina la Yesu Kristo, Amen.

 

No comments:

Post a Comment