Wednesday, April 24, 2013

Neno la leo

Zab 91:1-2 “Aketiye mahali pa siri pake aliye juu, Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi. Nitasema BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini”

TAFAKARI: Ukuu wa Mungu ni mkubwa kiasi kwamba hauwezi kulinganishwa na chochote. Nguvu zake ni za ajabu na hutushindia mengi na kutukinga na uovu wa aina yoyote.
SALA: Mwenyezi Mungu, wewe uliye mlinzi mkuu wa Israeli, kwa namna ya pekee naja mbele yako nikiomba ulinzi wa familia zetu dhidi ya ajali, magonjwa, majeraha na madhara ya aina yoyote ya mwili, akili na hisia. Naomba utuwezeshe kukimbilia daima vivulini mwa mbawa zako ili tuepukane na mabaya hayo. Moyo wangu umekutumaini wewe kwa makuu makubwa unayozidi kunitendea, nifanye BWANA nidumu daima katika pendo lako. Katika jina la Yesu Kristo naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment