Thursday, April 25, 2013

Neno la leo

Zab 6:9 “BWANA ameisikia dua yangu; BWANA atayatakabali maombi yangu”

TAFAKARI: Wakati mwingine tunakuwa tunajiuliza maswali mengi juu ya mambo yanayotokea. Ama pengine mtu anapitia majaribu kadhaa na kudiriki kushuku uwepo wa Mungu kama yupo ama ala. Mungu anasikia kila hitaji la mwanadamu, na hata majaribu mtu apitiayo ni sehemu moja wapo ya kupima imani ya mtu.
SALA: Mwenyezi Mungu, Baba wa Rehema, nasema asante kwa kusikia sala zangu. Kuna wakati nilikuwa nimechoka na kukata tama lakini wewe umenitoa kwenye mitego ya mwovu shetani. Sasa mimi ni kiumbe kipya na ninaukubali ukamilifu wako, Ee Mungu wa rehema. Naomba na kupokea katika jina la Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment