Monday, April 22, 2013

Neno la leo

Mit 5:21 “Kwa maana njia za mwanadamu zi mbele za macho ya BWANA, Na mienendo yake yote huitafakari”

TAFAKARI: Mungu huzichunguza njia za mwanadamu. Yawezekana mtu mwingine akafanya kitu kibaya akijiamini kwamba hakuna anaemuona. Lakini yeye aliye mbinguni huona na kuitafakari mienendo yetu wote.
SALA: Bwana Mungu, naomba nifundishe njia zako ili niweze kudumu na kuenenda katika njia hizo. Najua nimekuudhi na kukuangusha na hata nimejiangusha mwenyewe Mungu, lakini Bwana hujaniacha. Nichunguze Bwana, wala usinichoke zaidi nivute katika tumaini lako. Wewe uliyenifichia aibu katika yale niliyokutenda naomba unikumbatie kwa mbawa zako na kunisamehe. Katika jina la Yesu naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment