Friday, April 19, 2013

Neno la leo

Zab 51:10 “Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu”

TAFAKARI: Kwa jinsi Mungu anavyotuandalia makao yetu basi nasi hatuna budi kuandaa mahali pazuri akae hapo. Tumuombe atengeneze mioyo yetu iwe tayari na safi yenye kumtukuza yeye. Iwe mioyo yenye kukaribisha uwepo wa Mungu
SALA: Bwana Mungu, nataka moyo ambao unang’ang’ania ahadi zako. Naomba nipe roho iliyotulia ambayo itashikilia neno lako ndani yangu na unifanye niwe sehemu ambayo ina thamani ya kuitwa nyumba yako. Kadri ninavyoendelea mbele, Bwana nitakufikiria wewe ushiye ndani yangu ya kwamba unanineemesha kwa chakula chenye kunijenga kiroho kila siku. Naomba na kupokea katika jina mwanao Yesu Kristo, Amen.

No comments:

Post a Comment