Thursday, April 18, 2013

Neno la leo

Mit 17:24 “Hekima huwa machoni pake mwenye ufahamu; Bali macho ya mpumbavu huwa katika ncha za dunia”

TAFAKARI: Kuna wakati mtu huwa na shauku juu ya mipango aliyopanga. Kutaka kujua labda ningefanya hivi itakuwaje, je nitafanikisha, ama nini matokeo yake? Mwisho wa mambo hayo hukosa mwelekeo hivyo kuenenda katika njia ambazo hakuzifikiria.
SALA: Bwana Mungu naomba nisaidie niweze kuweka hekima yako na kuitazama kwa macho yaliyo wazi. Mara nyingine napoteza mtazamo wangu juu ya kipi ni chema na kipi kibaya, lakini nimekutumaini wewe kwa kuwa najua utaniokoa. Naomba nishike mabega yangu na uniongoze Bwana katika njia nzuri. Katika jina la Yesu, naomba na kupokea, Amen.

No comments:

Post a Comment